Saturday, March 8, 2014

wali wa asumini


Mchele kilo 1
Kuku mkubwa 1
Vitunguu maji kilo 2
Mayai 8
Samli kilo 1
Thomu gram 200
Tangawizi mbichi gram 50
Mdalasini gram 50
Hiliki gram 50
Bizari nzima kiasi
Siki kiasi
Mtindi painti 1
Tungule kilo 1
Zabibu nyeusi kiasi
1    Mkate kuku umwoshe umchemshe kwa maji na chumvi mpaka awive, kisha muepue.
2    Menya vitunguu uvioshe uvikate na uvigawe sehemu mbili. Sehemu moja uiweke, sehemu        ya pili vikaange mpaka       viwe vyekundu kama vya biriani. Kisha vichuje uitoe         samli yote, vitie katika sinia uvitandaze ili vipoe kwa kupata           upepo.
3   Chukua mdalasini, hiliki na bizari utwange pamoja, kisha uchunge unga laini. Saga         thomu na tangawizi mbichi. Saga      tungule.
4   Teleka sufuria tia samli ile ile iliyokaangiwa vitunguu halafu utie vile vitunguu         vilivyobakia uvikaange. Vikianza kuiva          tia viungo ulivyovitwanga na             kuvisaga. (Bakisha vitunguu na viungo kidogo). Tia vipande vya kuku, mtindi  siki na        supu ya kuku iliyobakia katika sufuria. Acha ichemke nyama pamoja na vitu vyote       mpaka libaki rojorojo.
5   Teleka maji, yakichemka tia chele. Ukiiva utoe uchuje yatoke maji yote.
6   Teleka tena sufuria utie samli kidogo utie na vile vitunguu ulivyovibakisha               uvikaange. Tia mdalasini nzima, kaanga          pamoja, tia na ule wali ukoroge           koroge ili uchanganyike na viungo. Kisha ufunike upalie moto.
7   Chemsha mayai yote uyamenye.
8   Wali ukishakauka utaupakua, lakini lazima itabidi utumie kombe au sahani kubwa           itakayoweza kuingia wali pamoja na vitu vyote. Kuupakua kwake kwanza utatia nusu ya       wali katika hiyo sahani, baadae utatia masalo na nyama yote, na mayai, kisha             utayafunika masalo kwa wali uliobakia. Mwisho utachukua vile vitunguu ulivyovikaanga     na ukavitandaza ili vipo, utavimwaga juu ya wali.Kwani ni kwa sababu ya hivi vitunguu     ndio maana ukaitwa wali wa asumini. Ukipenda utapamba chembe za zabibu juu yake.         ZABIBU HIZO Ziroweke kwanza ili zivimbe.

0 comments:

Post a Comment