Saturday, March 8, 2014

pishi la sambusa


Mahitaji
Unga wa ngano    ½
Viazi Ulaya    ¼kg 
Maji ya uvuguvugu kiasi
Kitunguu saumu kilichosagwa kijiko 1 kikubwa 
Tangawizi     kiasi
Pilipili mbuzi     1 (kama unatumia)
Vitunguu maji        3
Viungo            kiasi
Chumvi        kiasi
Njegere mbichi kikombe 1
Chumvi kiasi
Unga wa ngano vijiko 3 vya chakula.

Namna ya kutengeza

Chukua unga wa ngano ½ kg na kanda hadi ulainike kama unavyofanya kwa unga wa maandazi.
Baada ya hapo chukua mbogamboga zote katakata vipande vidogovidogo na kisha weka chumvi na baadaye viungo vya unga,kisha weka jikoni. 
Baaada ya dakika tano ipua na weka chini.

Gawa unga ulioukanda katika sehemu kumi. Tandaza kidogo,  kisha paka mafuta juu yake. Sukuma kama chapati,  kisha weka kwenye chuma cha kukaangia chapati bila ya kuweka mafuta.
Baada ya kubabua weka kwenye kibao cha chapati na kisha kata sehemu nne.
  
Chukua unga wa ngano vijiko 3 vya mezani na kisha tengeneza uji mzito kwa ajili ya kugandisha sambusa zako. 
Tengeneza umbo la koni kutoka kila kipande cha chapati ulichokata. Jaza mchanganyiko wa mbogamboga ndani yake. Funga sehemu ya juu, kwa kugandisha na uji uliotengeneza.

Fanya hivyo hadi chapatti zote ziishe. Chukua mafuta na weka jikoni, yakipata moto weka sambusa zako. Kaanga hadi ziwe rangi ya hudhurungi.


Ipua na chuja mafuta katika chujio la bati. Baada ya hapo sambusa zako zitakuwa tayari kuliwa.

0 comments:

Post a Comment