Saturday, March 8, 2014

biringanyi ya mbogamboga


Mahitaji:
  • ½ kg mchele wa basmati
  • Kitunguu maji kikubwa 1
  • Nyanya 1 kubwa
  • Karoti 1 kubwa
  • Njegere robo kikombe
  • Kiazi ulaya 1 kikubwa
  • Tangawizi za kusaga kijiko 1
  • Kitunguu swaumu cha kusaga kijiko 1
  • Karafuu kijiko 1
  • Majani ya kotimili fungu 1
  • Maziwa ya mtingi ¼ kikombe
  • Chumvi na pilipili kiasi
  • Unga wa dhani kijiko 1 cha mezani
  • Juisi ya limao kijiko 1 cha mezani
  • Mafua ¼ lita
Maandalizi:
  • Chemsha mchele na kisha weka pembeni
  • Osha mbogamboga zote isipokuwa vitunguu na nyanya
  • Changanya mtindi na tangawizi pamoja na kitunguu swaumu viache vikae kwa muda wa saa moja
  • Chukua sufuria weka mafuta na kisha kaanga vitunguu maji, weka nyanya, chumvi, kotimili na limao halafu weka karafuu na kanga hadi vichanganyike vizuri
  • Miminia mchanganyiko wa mtindi na baadaye weka pilipili na baadaye weka unga wa dhania
  • Chukua mchele uliochemshwa changanya na mchanganyiko huo
  • Palia moto juu ya chakula chako na acha kwa muda wa dakika 30
  • Baada ya hapo chakula chako cha biriani kitakuwa tayari kwa kuliwa

0 comments:

Post a Comment